Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

Wednesday, 6 November 2013

SIMBA YAITANDIKA ASHANTI UTD MABAO 4-2.


Mchezo wa ligi kuu ya Vodacom kati ya Simba na Ashanti UTD umemalizika hivi punde kwa Simba kupata ushindi wa mabao 4-2,mchezo huo ulipigwa kwenye dimba la uwanja wa taifa jijini Dar Es Salaam.
mabao ya Simba yamefungwa na Betram Mwombeki ( 2),Hamis Tambwe na Ramadhan Singano wakati yale ya Ashanti Utd yakiwekwa kimiani na Mkongwe Said Maulid na Hussein Said.

SERIKALI YAKUTANA NA UJUMBE WA SYMBION KUJADILI UJENZI WA KITUO CHA SOKA (SOCCER ACADEMY)




Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bi. Sihaba Nkinga, akisisitiza jambo, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam, alipokutana na ujumbe wa kampuni ya Symbion ya Marekani kujadili maandalizi ya ujenzi wa  kituo kikubwa cha maendeleo ya mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), ambayo itashirikiana na Club ya Sunderland ya Uingereza katika kuindesha Academy hiyo. Katika mpango  huo, Kampuni ya Symbion pia itajenga viwanja vya michezo (sports courts) eneo la Kidongo Chekundu. Mazungumzo hayo yamehusisha pia ujumbe wa viongozi kutoka Idara ya Michezo (hawapo pichani)